MKUTANO MKUU - OCTOBER 2019
Katika Misa na semina ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 10 wa Shirika. iliyoongozwa na Askofu tarehe 4.Oktoba. 2019
Makao Makuu ya Shirika, Kihesa Iringa
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kumi wa Shirika wakiwa na furaha tele baada ya kupata kitabu cha Sala za Shirika kilichochapishwa
upya baada ya kufanyiwa marekebisho kadhaa.
Padri Egidius wa Shirika la Damu Azizi ya Yesu Kristo katikati ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kumi wa Shirika. Ni
Mkufunzi wa pili aliyetoa Semina ya Maandalizi ya Mkutano.
Tukio ndani ya Mkutano Mkuu wa Kumi wa Shirika.
Pichani, Mama Mkuu CST akikabidhiwa na Askofu Mshumaa wa Jubilei uliowashwa tangu uzinduzi tarehe 4.Aprili. 2018 kwa lengo
la kuuzima alama ya kuhitimisha kilele cha Jubilei ya Novisiati miaka 50 tangu kuhamia Ulete. Misa iliadhimishwa
Ulete tarehe 22. Oktoba, siku ya kumbu kumbu ya
kifo cha Mons. Francesco Cagliero Mwanzilishi wa Shirika.
Wateresina, tujikumbushe tulikotoka, Tulipo na Tunakoelekea.
Zaidi ya uwepo wa Baba Askofu na Viongozi wa Shirika katika picha. mbele ni Wanovisi
ambao ni kielelezo halisi kuwa kila Mteresina alipitia hatua hiyo. Ni nafasi ya kujikumbusha mambo msingi tuliyopata katika vipindi
tofauti na makundi tofauti na ndizo nyenzo zetu muhimu katika utume wetu popote.
a
Matunda ya Mkutano Mkuu wa Kumi wa Shirika.
Katika picha hawa ni Mhashamu Askofu, Mapadri na Viongozi wapya na wa zamani wa shirika wakiwa mbele ya jiwe
lenye kumbu kumbu ya majina ya wasichana 12 waliojiunga kwa mara ya kwanza mwaka 1931.Leo shirika limekua mfano wa punje ya Haradali
Shukrani kwa Mungu na Kwa Mwanzilishi Mans Francesco Cagliero.